• HABARI MPYA

    Tuesday, February 27, 2018

    SIMBA NA MBAO FC KATIKA PICHA JANA TAIFA

    Mshambuliaji wa Simba SC, Mganda Emmanuel Okwi akimtoka beki wa Mbao FC, David Mwasa katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam. Simba ilishinda 5-0
    Mshambuliaji wa Mbao FC, Habib Kiyombo (katikati) akipambana kuwatoka wachezaji wa Simba, Yussuph Mlipili (kulia) na Mghana James Kotei (kushoto)
    Emmanuel Okwi akiwa ameanguka chini baada ya kupunguzwa kasi na beki wa Mbao FC, Boniphace Maganga
    Kiungo wa Simba, Muzamil Yassin akipasua katikati ya wachezaji wa Mbao
    Viungo, Yussuph Ndikumana (kushoto) na Muzamil Yassin (kulia) wakiwania mpira wa juu
    Beki wa Simba SC, Erasto Nyoni (kulia) akimgeuza Rajesh Kotecha wa Mbao FC 
    Beki wa Mbao FC, Amos Charles akimiliki mpira mbele ya kiungo wa Simba, Shiza Kichuya
    Kiungo wa Mbao FC, James Msuva akiudhibiti mpira dhidi ya beki wa Simba, Mghana, Asante Kwasi
    Kikosi cha Mbao FC kabla ya mchezo wa jana Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam 
    Kikosi cha Simba SC kilichoanza katika mechi ya jana Uwanja wa Taifa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA NA MBAO FC KATIKA PICHA JANA TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top