• HABARI MPYA

    Wednesday, March 21, 2018

    WAKALA WA BALOTELLI AWAKA KIJANA WAKE KUTOITWA TIMU YA TAIFA

    WAKALA wa Mario Balotelli, Mino Raiola amekasirishwa na kitendo cha mshambuliaji huyo kuachwa kwenye kikosi cha sasa cha Italia licha ya kuwa katika kiwango kizuri.
    Balotelli amefunga mabao 22 katika mechi 31 alizoichezea klabu yake, Nice katika Ligue 1 nchini Ufaransa msimu huu, lakini kocha wa muda wa Italia, Luigi Di Biagio hajamjumuisha kwenye kikosi kitakachomenyana na Argentina na England.
    Raiola, ambaye pia anamuwakilisha mchezaji ghali wa Manchester UnitedPaul Pogba, amesema hajafurahishwa na uamuzi wa kumuacha Balotelli kwenye mechi za kirafiki dhidi ya Argentina na England.

    Mario Balotelli has been left out of the most recent Italy squad by Luigi Di Biagio PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    "Tumesikitishwa na kutoitwa kwa Balotelli,"amesema Raiola. Tumesikitishwa pia na ufafanuzi tulioupokea, hadharani kwa sababu hatujazungumza na mtu hata mmoja,".
    Mshambuliaji huyo ameachwa baada ya kuitwa kwa wachezaji wapya kabisa The Azzuri, Patrick Cutrone na Federico Chiesa hawajaichezea hata mechi moja Italia. 
    Raiola amesema kwa rekodi yake msimu huu, Balotelli anastahili kuwemo kikosini kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2014.  
    "Kama Di Biagio anasema idadi (ya mabao) haihesabiwi kwa mshambuliaji, kisha milango ya timu ya taifa imefungwa kwa mchezaji kama yeye. Tatizo si kocha - ni mfumo wa soka. Tuna shirikisho linalofanya kazi bila mipango,"amesema.
    "Timu ya taifa lazima iwakilishwe na wachezaji bora, hivyo kama wachezaji wazuri hawaendi, basi hatujui vigezo,"ameongeza.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAKALA WA BALOTELLI AWAKA KIJANA WAKE KUTOITWA TIMU YA TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top