Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KLABU ya Fanja ya Oman, imefanikiwa kupata Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ya kiungo mkongwe kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa na sasa inaweza kuanza kumtumia katika Ligi ya nchi hiyo na Ligi ya Mabingwa Asia.
Akizungumza jana kutoka Oman, Ngassa alisema kwamba ITC yake imefika na Ijumaa alichezamechi yakeya kwanza wakifungwa 3-0 ugenini na Dhofar Uwanja wa Youth Complex mjini Salalah.
Ngassa amejiunga na Fanja kwa mkataba wa miaka miwili akitokea ya Free State Stars ya Afrika Kusini.
Mchezaji huyo wa zamani wa Toto Africans ya Mwanza, Kagera Sugar ya Bukoba, Yanga SC, Azam FC na Simba za Dar es Salaam anajiunga na wawakilishi hao wa Oman kwenye Ligi ya Mabingwa ya Asia, aliondoka Free State mwezi uliopita baada ya kuomba mwenyewqe kuvunja Mkataba.
Ngassa alijiunga na Free State Stars Mei mwaka jana akisajiliwa na kocha Mmalawi, Kinnah Phiri kwa mkataba wa miaka minne.
Hata hivyo, kocha aliyemsajili baba huyo wa Farida (9) na Faria (7) alifukuzwa baada ya miezi miwili tu na sasa tayari yuko Mbeya City ya Tanzania.
Katika kipindi cha mwaka mmoja wa kuwa Free State, Ngassa alifanya kazi na makocha wanne akiwemo huyu wa sasa, Mfaransa Denis Lavagne aliyeanza kazi Juni mwaka huu.
Wengine ni Mjerumani Ernst Middendorp aliyefanya kazi kati ya Septemba na Desemba 2015, Mtaliano Giovanni Solinas aliyefanya kazi kati ya Desemba na Mei 2016.
KLABU ya Fanja ya Oman, imefanikiwa kupata Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ya kiungo mkongwe kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa na sasa inaweza kuanza kumtumia katika Ligi ya nchi hiyo na Ligi ya Mabingwa Asia.
Akizungumza jana kutoka Oman, Ngassa alisema kwamba ITC yake imefika na Ijumaa alichezamechi yakeya kwanza wakifungwa 3-0 ugenini na Dhofar Uwanja wa Youth Complex mjini Salalah.
Ngassa sasa ameanza kucheza Ligi ya Oman |
Mchezaji huyo wa zamani wa Toto Africans ya Mwanza, Kagera Sugar ya Bukoba, Yanga SC, Azam FC na Simba za Dar es Salaam anajiunga na wawakilishi hao wa Oman kwenye Ligi ya Mabingwa ya Asia, aliondoka Free State mwezi uliopita baada ya kuomba mwenyewqe kuvunja Mkataba.
Ngassa alijiunga na Free State Stars Mei mwaka jana akisajiliwa na kocha Mmalawi, Kinnah Phiri kwa mkataba wa miaka minne.
Hata hivyo, kocha aliyemsajili baba huyo wa Farida (9) na Faria (7) alifukuzwa baada ya miezi miwili tu na sasa tayari yuko Mbeya City ya Tanzania.
Katika kipindi cha mwaka mmoja wa kuwa Free State, Ngassa alifanya kazi na makocha wanne akiwemo huyu wa sasa, Mfaransa Denis Lavagne aliyeanza kazi Juni mwaka huu.
Wengine ni Mjerumani Ernst Middendorp aliyefanya kazi kati ya Septemba na Desemba 2015, Mtaliano Giovanni Solinas aliyefanya kazi kati ya Desemba na Mei 2016.
0 comments:
Post a Comment