• HABARI MPYA

    Friday, October 21, 2016

    MOTO WAWAKA LIGI DARAJA LA KWANZA BARA

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    WAKATI mzunguko wa tano wa Ligi Daraja la Kwanza ukitarajiwa kuendelea kesho Jumamosi na keshokutwa Jumapili, Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeagiza makamishna na wakuu wa vituo kuzuia wachezaji wote ambao hawana leseni kutocheza.
    Hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14 (16), inayosema: “Wachezaji wote watatambulika kwa kutumia leseni zao zitakazotolewa na kuidhinishwa na TFF. Mchezaji yoyote ambaye hatakuwa na leseni hataruhusiwa kucheza katika mchezo husika.”

    Kipindi cha dharura amvacho TFF ilikitoa ni kwa mizunguko mitatu ya mwanzo, lakini taarifa za makamishna zinaonyeha kuwa raundi ya nne bado kuna timu zilikuwa zinatumikia leseni za muda ilihali walikwisha kutaarifiwa kuwa leseni zao ziko tayari na wao wanakwama kuzifuata hapa TFF. Kuanzia sasa hakuna sababu yoyote itakayotolewa na ikaeleweka kwa mchezaji ambaye hatakuwa na leseni.
    Kwa mujibu wa ratiba ya Ligi Daraja la Kwanza, michezo ya Kundi A kesho itakuwa ni kati ya Pamba ya Mwanza na African Sports ya Tanga kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati Dar es Salaam kutakuwa na ‘Mbezi Derby’ ambako Kiluvya United itacheza na Mshikamano kwenye Uwanja wa Karume, Ilala.
    Katika kundi hilo, Friends Rangers pia ya Dar es Salaam, itacheza na Lipuli ya Iringa Jumatatu kwenye uwanja huo wa Karume, Dar es Salaam wakati Jumanne Oktoba 25, 2016 Polisi Dar itacheza na Ashanti United ya Ilala. Mchezo huo pia utafanyika Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
    Kundi B kutakuwa na mchezo kati ya Mbeya Warriors ya Mbeya na Coastal Union ya Tanga; Kemondo itacheza na Mlale ilihali Polisi Moro itacheza na Kurugenzi ya Iringa wakati Jumapili Oktoba 23 KMC ya Kinondoni, Dar es Salaam itacheza na Mji Njombe.
    Kwa upande wa Kundi C michezo yote minne itachezwa kesho Oktoba 22, mwaka huu ambako Singida United itacheza na Polisi Dodoma kwenye Uwanja wa Namfuta mjini Singida; Rhino itapambana na Alliance ya Mwanza kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora huku Mgambo JKT itakuwa mwenyeji wa Mvuvumwa ya Kigoma kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MOTO WAWAKA LIGI DARAJA LA KWANZA BARA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top