• HABARI MPYA

    Wednesday, June 22, 2016

    RONALDO APIGA MBILI, LAKINI URENO YATOLEWA EURO 2016

    Nyota wa Ureno, Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungi timu yake mabao mawili ikitoa sare ya 3-3 na Hungary katika mchezo wa Kundi F Euro 2016 usiku huu Uwanja wa Parc Olympique Lyonnais mjini Decines-Charpieu, Ufaransa. Bao lingine la Ureno limefungwa na Nani, wakati ya Hungary yamefungwa na Zoltan Gera na Balazs Dzsudzsak mawili. Kwa matokeo hayo Hungary inamaliza kileleni mwa kundi hilo kwa pointi zake tano sawa na Iceland inayomaliza nafasi ya pili na zote zinakwenda hatua ya 16 Bora, huku Ureno iliyomaliza na pointi tatu ikitolewa  PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    Kiungo wa Austria, Julian Baumgartlinger (kushoto) akiwa ameanguka chini baada ya kulambwa chenga na Gylfi Sigurdsson (kulia) katika mchezo wa Kundi F Euro 2016 Uwanja wa Stade de France mjini Paris, Ufaransa. Iceland ilishinda 2-1  PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO APIGA MBILI, LAKINI URENO YATOLEWA EURO 2016 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top