• HABARI MPYA

    Monday, June 27, 2016

    KAPTENI BOCCO ANAVYOJIFUA KUJIANDAA NA MSIMU MPYA

    Nahodha wa Azam FC, John Raphael Bocco 'Adebayor' akifanya mazoezi ya kukimbia katika ufukwe wa bahari ya Hindi eneo la Africana, Mbezi mjini Dar es Salaam kujiandaa na msimu mpya
    Mshambuliaji huyo ana wiki sasa akifanya mazoezi binafsi kujiweka fiti kabla ya kuingia kwenye programu za maandalizi ya msimu mpya za timu yake
    Bocco amesema asubuhi anafanya mazoezi ufukweni, mchana gym na jioni anacheza mpira na timu ya mtaani kwake
    Bocco amesema nia yake ni kuhakikisha msimu ujao anarejesha makali yake na kuisaidia timu yake
    Ikumbukwe msimu uliopita Bocco hakufanya vizuri sana kutokana na kuandamwa na maumivu
    Bocco pia ni mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania na Nahodha wa kikosi cha CHAN
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAPTENI BOCCO ANAVYOJIFUA KUJIANDAA NA MSIMU MPYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top