• HABARI MPYA

    Wednesday, November 08, 2017

    ABRAMOVICH AANZA KUMCHUNGUZA CONTE UGOMVI NA WACHEZAJI

    MMILIKI wa Chelsea, Mrusi Roman Abramovich ameanza uchunguzi wa kinachoendelea katika mahusiano ya kocha Mtaliano Antonio Conte na beki Mbrazil, David Luiz – kufuatia kujiuzulu kwa Mkurugenzi wa Ufundi, Mnigeria Michael Emenalo juzi.
    Conte anadaiwa kumuweka benchi Luiz kwenye mchezo uliopita The Blues wakishinda 1-0 dhidi ya Manchester United – kwa kuhoji mambo fulani fulani ya kiufundi mazoezini kuelekea kwenye mechi hiyo ya Ligi Kuu ya England.
    Na hii ni kufuatia hali ya wasiwasi inayoibuka juu ya tabia ya Conte kugombana na wachezaji, baada ya awali kuhitilafiana pia na Diego Costa.

    Mrusi Roman Abramovich ameanza uchunguzi wa mahusiano baina ya kocha Antonio Conte na wachezaji Chelsea PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ABRAMOVICH AANZA KUMCHUNGUZA CONTE UGOMVI NA WACHEZAJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top