• HABARI MPYA

    Monday, March 31, 2014

    TFF YATOA RAMBIRAMBI MSIBA WA DK HEMED MZIRAY

    Na Boniface Wambura, Dar es Salaam
    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha daktari wa tiba ya michezo, Dk. Hemed Mziray kilichotokea juzi jijini Dar es Salaam.
    Dk. Mziray ambaye alikuwa mfanyakazi wa Hospitali ya Manispaa ya Temeke na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Tiba ya Michezo Tanzania (TASMA) amesafirishwa kwenda kwao mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.
    Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Dk. Mziray ameshirikiana na TFF na wadau wengine wa mpira wa miguu katika masuala ya tiba na uongozi.
    Rais wa TFF, Jamal Malinzi katikati

    Alikuwa kiungo kati ya Uwanja wa Taifa ambapo mechi za kimataifa, za ligi na za kirafiki zimekuwa zikichezwa na Hospitali ya Temeke kwa wagonjwa wanaohitaji huduma zaidi, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
    TFF imetoa pole kwa familia ya marehemu Dk. Mziray, TASMA na wafanyakazi wa Hospitali ya Temeke na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Pia TFF inatoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake. Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF YATOA RAMBIRAMBI MSIBA WA DK HEMED MZIRAY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top