• HABARI MPYA

    Friday, March 21, 2014

    MAN UNITED NA BAYERN, BARCA NA MADRID ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA

    KLABU ya Manchester United itakutana na mabingwa watetezi, Bayern Munich katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya droo iliyomalizika kupangwa muda huu mjini Nyon, Uswisi.
    Timu nyingine pekee ya England iliyobaki katika michuano hiyo, Chelsea imepelekwa kwa mabingwa wa Ufaransa, Paris Saint-Germain baada ya kuchaguliwa na Luis Figo.
    Mechi nyingine ni kati ya timu za Hispania tupu Barcelona na Atletico Madrid wakati Real Madrid itamenyana na Borussia Dortmund ya Ujerumani.

    Mwali: Taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya likiwa mjini Nyon, Uswisi wakati wa upangaji wa droo ya Robo Fainali

    ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA 2014

    Barcelona vs Atletico Madrid
    Real Madrid vs Borussia Dortmund
    Paris Saint-Germain vs Chelsea
    Manchester United vs Bayern Munich
    Mechi za kwanza zitachezwa Aprili 1 na 2, wakati marudiano itakuwa Aprili 8 na 9.
    In the mix: Wayne Rooney and Manchester United are outsiders for the competition after scraping through
    Mtihani mgumu: Wayne Rooney na Manchester United watatapambana na mabingwa watetezi, Bayern Munich
    Happy? Samuel Eto'o and Chelsea eased past Galatasaray in the round of 16 after a 2-0 win at Stamford Bridge
    Furaha? Samuel Eto'o na Chelsea waliitoa Galatasaray Hatua ya 16 Bora
    Big boys: Real Madrid's Cristiano Ronaldo (right) and Gareth Bale are looking to deliver another trophy
    Majina makubwa: Wachezaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo (kulia) na Gareth Bale kushoto
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED NA BAYERN, BARCA NA MADRID ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top