• HABARI MPYA

    Friday, March 28, 2014

    NATURE, PROFESA JAY NA JAY MOE WATOA WIMBO KWA PAMOJA UITWAO JWTZ, WATUMIA ZANA HALISI ZA JESHI KATIKA VIDEO YAO

    Na Dina Ismail, Dar es Salaam
    WASANII watatu wakongwe na maarufu wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Juma Mchopanga ‘Jay Moe’, Juma Kassim ‘Nature’ na Joseph Haule ‘Profesa Jay’ wamerekodi kwa pamoja wimbo uitwao JWTZ.
    Wimbo huo umerekodiwa kwa sauti na video katika studio za Williamz Visions chini ya mtayarishaji Mike Mwakatundu ‘Mike T’.
    Profesa Jay akiimba katika moja ya maonyesho Dar es Salaam

    Mike T maarufu kama Mnyalu, ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, yeye anakuwa muongozaji wa kwanza wa video au filamu Tanzania kupata fursa ya kutumia vifaru, ndege, helikopta na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) katika kazi zake.
    “Naamini kwa kumtanguliza Mungu kila kitu kinawezekana, baada ya yote, naamini magwiji hao wamefanya kweli,”amesema Mike T, ambaye pia ni gwiji wa Bongo Fleva.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NATURE, PROFESA JAY NA JAY MOE WATOA WIMBO KWA PAMOJA UITWAO JWTZ, WATUMIA ZANA HALISI ZA JESHI KATIKA VIDEO YAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top