• HABARI MPYA

    Sunday, March 23, 2014

    EL CLASICO UHONDO WAONGEZEKA, BENZEMA NA PIQUE WAREJEA KUZIONGEZEA NGUVU REAL MADRID NA BARCA ZIKIMENYANA LEO LA LIGA

    TIMU za Barcelona na Real Madrid zote zimeongezewa nguvu kuelekea mchezo wa leo usiku wa El Clasico kufuatia habari kwamba Gerard Pique na Karim Benzema watakuwepo kwenye mechi hiyo itakayopigwa Uwanja wa Santiago Bernabeu, Madrid.
    Beki Pique hakuwepo wakati Barca inashinda 7-0 dhidi ya Osasuna kutokana na maumivu ya kifundo cha mguu wa kulia, lakini alirejea mazoezini Jumatatu wiki hii.
    Pamoja na hayo, Carles Puyol, ambaye ataondoka Nou Camp mwishoni mwa msimu, atakosa mchezo ambao ungekuwa wa mwisho kwake dhidi ya Real kutokana na maumivu ya goti.
    Atakosekana: Carles Puyol anatarajiwa kuikosa 'El Clasico' yake ya mwisho akiwa na jezi ya Barcelona kutokana na maumivu ya goti
    Jokers: Neymar and Jordi Alba lark around during Barcelona's training session on Saturday
    Neymar na Jordi Alba wakiwa mazoezini na wenzao wa Barcelona jana tayari kwa mchezo wa leo
    High spirits: Midfielder Alex Song jokingly pushes Neymar to the ground as Alba watches on
    Kiungo Alex Song akitaniana na Neymar kwa kumsukuma uwanjani huku Alba akitazama
    All smiles: Gerard Pique attended his partner Shakira's album launch in Barcelona on Friday
    Wote wanatabasamu: Gerard Pique alihudhuria uzinduzi wa albamu ya mpenzi wake, Shakira mjini Barcelona Ijumaa

    Wakati huo huo, mwanasoka wa kimataifa wa Ufaransa, Karim Benzema anatarajiwa kurejea kwenye kikosi cha Los Blancos baada ya kukosa mechi timu yake ikishinda mabao 3-1 dhidi ya Schalke katika Ligi ya Mabingwa Jumanne.
    Mshambuliaji huyo wa zamani wa Lyon alirejea kwenye kikosi cha kocha Carlo Ancelotti jana baada ya kuumia siku Madrid ikiilaza 1-0 Malaga ugenini.
    Vinara wa La Liga, Real wanaingia kwenye mchezo wa leo wakiwa wanawazidi kwa pointi nne wapinzani wao hao, Barcelona walio katika nafasi ya tatu nyuma ya Atletico wanaowazidi pia pointi tatu.
    He's in fashion: Cristiano Ronaldo, wearing rather usual head gear, trains with Gareth Bale
    Wakali wawili: Cristiano Ronaldo akifanya mazoezi na Gareth Bale jana tayari kwa mchezo wa leo
    Practice makes perfect: League leaders Real Madrid pass the ball around during Saturday's training session
    Wachezaji wa Real Madrid mazoezini jana
    Star man: Lionel Messi climbs the steps at Barcelona's Sports Centre on Saturday
    Nyota kweli: Lionel Messi akishuka Uwanja wa mazoezi wa Barcelona, Sports Centre jana kwenda kujifua kwa ajili ya mechi ya leo
    In the hotseat: Barcelona boss Gerardo Martino (left) and Madrid manager Carlo Ancelotti go head-to-head on Sunday night
    In the hotseat: Barcelona boss Gerardo Martino (left) and Madrid manager Carlo Ancelotti go head-to-head on Sunday night
    Wataalamu: Kocha wa Barcelona, Martino (kushoto) na wa Madrid, Ancelotti nani ataipa ushindi timu yake leo?
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: EL CLASICO UHONDO WAONGEZEKA, BENZEMA NA PIQUE WAREJEA KUZIONGEZEA NGUVU REAL MADRID NA BARCA ZIKIMENYANA LEO LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top