• HABARI MPYA

    Sunday, March 30, 2014

    JOHN BOCCO AISOGEZA AZAM FC JIRANI KABISA NA UBINGWA

    Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
    AZAM FC imezidi kupiga kasi katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya jioni hii kukiagusha kigogo, SImba SC kwa mabao 2-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Matokeo hayo yanaifanya Azam itemize pointi 53 baada ya mechi 23, wakati Yanga SC inabaki na pointi zake 46 baada ya mechi 22.
    Shujaa; Mfungaji wa bao la ushindi la Azam FC kulia akipiga shuti pembeni ya kiungo wa Simba SC, Jonas Mkude

    Shukrani kwake mshambuliaji John Raphael Bocco ‘Adebayor’ aliyefunga bao la ushindi dakika ya 56 kwa kichwa kufuatia pasi ya tika tak ya Kipre Herman Tchetche. 
    Tayari timu hizo zilikuwa zimekwishafungana bao 1-1 hadi mapumziko, Azam FC wakitangulia kupata bao lao kupitia kwa Khamis Mcha Vialli dakika ya 16 na Simba SC wakisawazisha kupitia kwa Joseph Owino dakika ya 45 na ushei.
    Mcha alifunga bao kwa urahisi baada ya kutengewa mpira kwa kifua na Kipre Tchetche aliyepokea krosi Gardiel Michael- ambaye naye alipata pasi ya John Bocco aliyefanya kazi kubwa ya kupanda na mpira kutokea nyuma.
    Owino alifunga kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na winga machachari, Ramadhani Singano ‘Messi’.
    Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Ivo Mapunda, William Lucian ‘Gallas’, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Henry Joseph/Abdulhalim Humud dk66, Haruna Chanongo, Amisi Tambwe, Uhuru Suleiman na Ramadhani Singano ‘Messi’.
    Azam FC; Aishi Manula, Erasto Nyoni, Gardiel Michael, Aggrey Morris, David Mwantika, Kipre Balou, Himid Mao/Bryson Raphael dk75 , Salum Abubakar ‘Sure Boy’, John Bocco ‘Adebayor’, Kipre Tchetche/Brian Umony dk80 na Khamis Mcha ‘Vialli’/Kevin Friday dk55.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JOHN BOCCO AISOGEZA AZAM FC JIRANI KABISA NA UBINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top