• HABARI MPYA

    Tuesday, March 25, 2014

    OZIL AENDA KUJIRUSHA KWENYE PATI LA DEMU WAKE SAA CHACHE BAADA YA ARSENAL KULA 6-0 ZA CHELSEA

    SAA chache baada ya kipogo cha mabao 6-0 amnbacho Arsenal ilikipata kutoka kwa Chelsea Jumamosi katika Ligi Kuu ya England, baadhi ya wachezaji wa The Gunners walikwenda kusherehekea sherehe ya kuzaliw akwa demu wa Mesut Ozil.
    Picha zilizovuja kutoka mitandao ya kijamii Jumatatu jioni, zinawaonyesha Ozil, Nicklas Bendtner na Bacary Sagna wakijirusha kwenye pati hilo Jumamosi jioni Mandy Capristo akisherehekea kutimiza miaka 24.
    Ozile 'amekufa ameoza' kwa mlimbwende huyo na wakati fulani alipokuwa Real Madrid aliwahi kuambiwa kimwana huyo anamaliza soka yake.
    Pati baada ya kipigo: Demu wa Ozil ameposti picha hii katika ukurasa wa Instagram. Ozil, Bendtner na Sagna wote wanatabasamu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: OZIL AENDA KUJIRUSHA KWENYE PATI LA DEMU WAKE SAA CHACHE BAADA YA ARSENAL KULA 6-0 ZA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top