• HABARI MPYA

    Friday, February 24, 2017

    MAN UNITED YAPELEKWA URUSI 16 BORA EUROPA LEAGUE, SAMATTA...

    Manchester United ya Jose Mourinho itamenyana na Rostov ya Urusi katika hatua ya 16 Bora michuano ya Europa League PICHA ZAIDI GONGA HAPA  


    RATIBA 16 BORA EUROPA LEAGUE 

    Celta Vigo vs Krasnodar
    APOEL vs Anderlecht
    Schalke vs Borussia Monchengladbach
    Lyon vs Roma
    Rostov vs Manchester United
    Olympiacos vs Besiktas
    Gent vs Genk
    Copenhagen vs Ajax 
    VIGOGO wa England, Manchester United watamenyana na Rostov katika hatua ya 16 Bora michuano ya Europa League.
    United iliingia hatua ya 16 kwa kishindo, baada ya kuitandika jumla ya mabao 4-0 St Etienne katika raundi ya kwanza ya mchujo.
    Mechi mbili zitachezwa kati ya Machi 9 na Machi 16, mwaka huu baina ya timu hizo. Timu ya Jose Mourinho watakuwa safari ngumu ya Urusi, siku nne kabla ya kukutana na Chelsea katika Robo Fainali ya Kombe la FA. 
    KRC Genk ya Nahodha wa Tanzania, Mbwana Samatta imeangukia kwa wapinzani wao wa Ubelgiji, Gent, wakati Schalke itamenyana na wapinzani wao wa Bundesliga, Borussia Monchengladbach.
    Mechi nyingine Celta Vigo ya Hispania itamenyana na Krasnodar, APOEL ya Cyprus na Anderlecht ya Ubelgiji, Lyon ya Ufaransa na Roma ya Italia, Olympiacos ya Ugiriki na Besiktas ya Uturuki na Copenhagen ya Sweden dhidi ya Ajax ya Uholanzi. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YAPELEKWA URUSI 16 BORA EUROPA LEAGUE, SAMATTA... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top