• HABARI MPYA

    Thursday, December 12, 2019

    JESUS APIGA HAT TRICK, MAN CITY YAICHAPA DINAMO ZAGREB 4-1

    Gabriel Jesus akishangilia baada ya kuifungia Manchester City mabao matatu dakika za 34, 50 na 54 katika ushindi wa 4-1 dhidi ya wenyeji, Dinamo Zagreb kwenye mchezo wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Maksimir, Zagreb. Bao la nne la Man City lilifungwa na Phil Foden dakika ya 84, wakati la Dinamo Zagreb lilifungwa na Daniel Olmo dakika ya 10. Manchester City imeongoza kundi hilo kwa pointi zake 14, ikifuatiwa na Atalanta iliyomaliza na pointi saba baada ya kuwafunga wenyeji Shakhtar Donetsk 3-0 jana na zote zinafuzu hatua ya 16 Bora 


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JESUS APIGA HAT TRICK, MAN CITY YAICHAPA DINAMO ZAGREB 4-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top