• HABARI MPYA

    Wednesday, December 11, 2019

    FATI AFUNGA BAO LA REKODI BARCA YAICHAPA INTER MILAN 2-1

    Kinda wa miaka 17 wa Guinea-Bissau Ansu Fati akipongezwa na wenzake baada ya kuifungia Barcelona bao la pili dakika ya 86 ikiwalaza wenyeji, Inter Milan 2-1 katika mchezo wa Kundi F Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Giuseppe Meazza mjini Milan akiweka rekodi ya mchezaji mwenye mdogo zaidi kufunga kwenye michuano hiyo kihistoria. Bao la kwanza la Barca ambayo kwa ushindi huo inatinga hatua ya 16 Bora ikiungana naBorussia Dortmund, lilifungwa na Carles Perez dakika ya 23, wakati la wenyeji lilifungwa na Romelu Lukaku dakika ya 44 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FATI AFUNGA BAO LA REKODI BARCA YAICHAPA INTER MILAN 2-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top