• HABARI MPYA

    Sunday, October 27, 2019

    REFA AKATAA BAO LA ARSENAL YATOA SARE 2-2 NA CRYSTAL PALACE

    Beki Mgiriki wa Arsenal, Sokratis Papastathopoulos akilalamika baada ya kukataliwa bao lake dakika za mwishoni kufuatia refa Martin Atkinson kutazama marudio ya picha za video (VAR) wakitoa sare ya 2-2 na Crystal Palace kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Emirates. Mabao ya Arsenal yamefungwa na Papastathopoulos dakika ya saba na beki mwingine, Mbrazil David Luiz dakika ya tisa, wakati ya Crystal Palace yamefungwa na Luka Milivojevic kwa penalti dakika ya 32 na Jordan Ayew dakika ya 52 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REFA AKATAA BAO LA ARSENAL YATOA SARE 2-2 NA CRYSTAL PALACE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top