• HABARI MPYA

    Wednesday, October 30, 2019

    AISHI KUDAKA MECHI YA 100 LEO TANGU ASAJILIWE SIMBA JUNI 2017

    Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
    LIGI Kuu ya Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo kwa mechi saba kuchezwa kwenye viwanja tofauti, ingawa macho na masikio ya wengi yataelekezwa Uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga.
    Huko, mabingwa watetezi na timu bora kwa sasa nchini, Simba SC watakuwa wanamenyana na wenyeji, Mwadui FC kuanzia Saa 10:00 jioni.
    Na hapana shaka, kocha Mbelgiji Patrick Aussems ataendelea kumuamini mlinda mlango wake namba moja, Aishi Salum Manula kuwa kumuanzisha. 
    Aishi Manula anatarawa kusimama kwenye lango la Simba kwa mara ya 100 leo

    Na kama ataanzishwa leo, Aishi atakuwa anasimama kwenye lango la Simba kwa mara ya 100 tangu asajiliwa kutoka timu iliyomuibua na kumkuza kisoka, Azam FC Juni mwaka 2017.
    Hapana shaka mechi 100 ndani ya miaka miwili ni kielelezo tosha cha namna Aishi, ambaye pia ni kipa bora wa Ligi Kuu mara tatu mfululizo anavyotumika Simba SC akiwa chachu ya mafanikio ya timu katika misimu hii miwili.
    Mbele na nyuma, kushoto na kulia ni Aishi peke yake – huyo ndiye kipa bora wa Ligi Kuu na nchi kwa ujumla, haijalishi kwa sasa anafungiwa vioo na kocha Mrundi wa timu ya taifa ya Tanzania, Etienne Ndayiragije. 
    Uhodari wake ndiyo umeirejesha Simba SC katika ramani ya soka Afrika baada ya msimu uliopita kuiwezesha kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa na kuivusha hadi Robo Fainali ambako ilitolewa na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
    Katika mechi zote 99 alizodaka hadi sasa Aishi amesimama langoni mara 59 bila kuruhusu bao Simba SC na kwa ujumla amefungwa mabao 59, akiiongoza timu kushinda mechi 67, kufungwa 12 na sare 20.
    Akiwa ametoka kutimiza umri wa miaka 24 Septemba 13, mwaka huu, Aishi tayari ameingia kwenye orodha ya makipa bora kuwahi kutokea siyo tu katika klabu yake, Simba bali hata na nchini kwa ujumla na sasa anawania kuweka rekodi zaidi ili kudhihirisha ubora wake. 
    Huyo ndiye kipa aliyeiwezesha Taifa Stars kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) Juni mwaka huu nchini Misri.   
    Kila la heri Aishi Salum Manula kuelekea mechi yako ya 100 Simba SC ikimenyana na Mwadui FC leo Uwanja wa Kambarage.
    Aishi Manula amesimama langoni mara 59 bila kuruhusu bao Simba SC katika 99 alizodaka hadi sasa 

    REKODI YA AISHI MANULA SIMBA
    Simba 1-0 Rayon Sport (Hakufungwa Kirafiki Simba Day Taifa)
    Simba 0-0 Mlandege FC  (Hakufungwa Kirafiki Amaan, Zbar)
    Simba 0-0 (5-4 penalti) Yanga (Hakufungwa Ngao ya Jamii, Taifa Penalti)
    Simba SC 7-0 Ruvu Shooting (Hakufungwa Ligi Kuu Uhuru)
    Simba 0-0 Azam FC (Hakufungwa Ligi Kuu Chamazi)
    Simba SC 3-0 Mwadui (Hakufungwa Ligi Kuu Uhuru)
    Simba 2 – 2 Mbao FC (Alifungwa mbili Ligi Kuu Kirumba, Mwanza)
    Simba 0-0 Milambo (Aliingia, hakufungwa Kirafiki A. Mwinyi, Tabora)
    Simba 2-1 Stand United (Alifungwa moja Ligi Kuu Shinyanga)
    Simba SC 1-1 Mtibwa Sugar (Alifungwa moja Ligi Kuu Uhuru)
    Simba SC 4-0 Njombe Mji (Hakufungwa Ligi Kuu Uhuru)
    Simba 1-1 Yanga (Alifungwa moja Ligi Kuu Uhuru)
    Simba 1-0 Mbeya City (Hakufungwa Ligi Kuu Sokoine)
    Simba 1-0 Tanzania Prisons (Hakufungwa Ligi Kuu Sokoine)
    Simba 1-1 Lipuli FC (Alifungwa moja Ligi Kuu Uhuru)
    Simba 1-1 (Penalti 3-4) Green Warriors (Alifungwa moja na penalti nne Kombe la TFF Chamazi)
    Simba 2-0 Ndanda FC (Hakufungwa Ligi Kuu Nangwanda)
    Simba 4-0 Singida United  (Hakufungwa Ligi Kuu Uhuru)
    Simba 2-0 Kagera Sugar  (Hakufungwa Ligi Kuu Kaitaba)
    Simba 4-0 Maji Maji FC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba 3-0 Ruvu Shooting FC (Hakufungwa Ligi Kuu Uhuru)
    Simba 1-0 Azam FC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba 4-0 Gendarmerie Tnare  (Hakufungwa, Kombe la Shirikiaho Kuu Taifa)
    Simba 2-2 Mwadui FC (Alifungwa mbili Ligi Kuu Kambarage)
    Simba 1-0 Gendarmerie Tnare  (Hakufungwa – Kombe la Shirikisho Djibouti)
    Simba 5-0 Mbao FC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba 3-3 Stand United (Alifungwa zote tatu Ligi Kuu Taifa)
    Simba 2-2 Al Masry  (Alifungwa mbili moja kwa penalti Kombe la Shirikisho Taifa)
    Simba 0-0 Al Masry  (Hakufungwa Kombe la Shirikisho Port Said)
    Simba 2-0 Njombe Mji FC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa Njombe)
    Simba SC 1-0 Mtibwa Sugar (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa) 
    Simba 3-1 Mbeya City  (Alifungwa moja Ligi Kuu Taifa)
    Simba 2-0 Tanzania Prisons  (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba 1-1 Lipuli FC  (Alifungwa moja, Ligi Kuu Samora)
    Simba 1-0 Yanga SC (Hakufungwa, Ligi Kuu Taifa)
    Simba 1-0 Ndanda FC  (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba 1-0 Singida United  (Hakufungwa Ligi Kuu Namfua)
    Simba 0-0 (3-2 Penalti) Kariobangi Sharks  (Hakufungwa, akaokoa penalty moja SportPesa SuperCup Nakuru)
    Simba 0-0 (5-4 Penalti) Kakamega Homeboys (Hakufungwa SportPesa SuperCup Nakuru)
    Simba 0-2 Gor Mahia (Alifungwa mbili SportPesa SuperCup Nakuru)
    Simba SC 1-1 F.C.E KSAIFA ya Palestina (Hakufungwa kirafiki ziara ya Uturuki)
    Simba SC 3-1 MC Oujder ya Morocco (Hakufungwa Kirafiki ziara ya Uturuki)
    Simba SC 1-1 Asante Kotoko ya Ghana (Alifungwa moja Kirafiki Simba Day Taifa)
    Simba SC 2-1 Arusha United (Alifungwa moja Kirafiki Uwanja wa S.A. Abeid, Arusha)
    Simba SC 2-1 Mtibwa Sugar (Alifungwa moja Ngao ya Jamii Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza)
    Simba SC 1-0 Tanzania Prisons (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 2-0 Mbeya City (Hakufungwa, Ligi Kuu Taifa alitoka baada ya kuumia dk53 akaingia Abdul Salim)
    Simba SC 0-0 Ndanda FC (Hakufungwa Ligi Kuu Mtwara)
    Simba SC 0-1 Mbao FC (Alifungwa moja kwa penalti Ligi Kuu Mwanza)
    Simba SC 3-1 Mwadui FC (Alifungwa moja Ligi Kuu Shinyanga)
    Simba SC 0-0 Yanga SC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 2-1 African Lyon (Alifungwa moja Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 3-0 Stand United (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 5-1 Alliance FC (Alifungwa moja Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 5-0 Ruvu Shooting FC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 2-0 JKT Tanzania (Hakufungwa Ligi Kuu Mkwakwani)
    Simba SC 0-0 Lipuli FC (Hakufungwa Ligi Kuu Uwanja wa Taifa)
    Simba SC 4-1 Mbabane Swallows (Alifungwa moja Ligi ya Mabingwa Afrika Taifa)
    Simba SC 4-0 Mbabane Swallows (Hakufungwa Ligi ya Mabingwa Afrika Manzini)
    Simba SC 1-2 Nkana FC (Alifungwa mbili Ligi ya Mabingwa Afrika Kitwe) 
    Simba SC 3-1 Nkana FC (Alifungwa moja Ligi ya Mabingwa Afrika Taifa)
    Simba SC 3-0 Singida United (Hakufungwa Ligi Kuu Uwanja wa Taifa)
    Simba SC 1-0 KMKM (Hakufungwa Kombe la Mapinduzi, Zanzibar)
    Simba SC 3-0 JS Saoura (Hakufungwa Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika Taifa)
    Simba SC 0-5 AS Vita (Alifungwa tano Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika Kinshasa) 
    Simba SC 2-1 AFC Leopards (Alifungwa moja SportPesa Super Cup Taifa)
    Simba SC 1-2 Bandari FC (Alifungwa mbili SportPesa Super Cup Taifa)
    Simba SC 0-5 Al Ahly (Alifungwa tano Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika Cairo)
    Simba SC 3-0 Mwadui FC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 1-0 Al Ahly (Hakufungwa Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika Dar) 
    Simba SC 1-0 Simba SC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 3-0 African Lyon (Hakufungwa Ligi Kuu Sheikh Amri Abeid)
    Simba SC 3-1 Azam FC (Alifungwa moja Ligi Kuu Taifa) 
    Simba SC 3-1 Lipuli FC (Alifungwa moja Ligi Kuu Samora)
    Simba SC 2-0 Stand United (Hakufungwa Ligi Kuu Kambarage)
    Simba SC 0-2 JS Saoura (Alifungwa mbili Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika Bechar) 
    Simba SC 2-1 AS Vita (Alifungwa moja Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika Dar) 
    Simba SC 0-0 TP Mazembe (Hakufungwa Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika Dar)
    Simba SC 1-4 TP Mazembe (Alifungwa nne Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika Lubumbashi)
    Simba SC 2-1 Coastal Union (Alifungwa moja Ligi Kuu Mkwakwani, Tanga)
    Simba SC 1-2 Kagera Sugar (Alifungwa moja, Ligi Kuu Kaitaba, Bukoba) 
    Simba SC 2-0 Alliance FC (Hakufungwa Ligi Kuu Kirumba, Mwanza) 
    Simba SC 2-1 KMC (Alifungwa moja Ligi Kuu Kirumba, Mwanza)
    Simba SC 1-0 Tanzania Prisons (Hakufungwa Ligi Kuu, Sokoine)
    Simba SC 8-1 Coastal Union (Alifungwa moja Ligi Kuu, Uhuru)
    Simba SC 0-1 Kagera Sugar (Alifungwa moja Ligi Kuu, Uhuru)
    Simba SC 0-0 Azam FC (Hakufungwa Ligi Kuu, Uhuru)
    Simba SC 3-0 Mtibwa Sugar (Hakufungwa Ligi Kuu, Uhuru)
    Simba SC 2-0 Ndanda FC (Hakufungwa Ligi Kuu, Uhuru)
    Simba SC 4-5 Sevilla (Alifungwa moja akampisha Deo Munishi dk46 akafungwa nne Kirafiki Taifa)
    Simba SC 4-0 Orbit Tvet (Hakufungwa, alimpisha Benno Rusternburg)  
    Simba SC 1-1 UD Songo (Alifungwa moja Ligi ya Mabingwa Taifa)
    Simba SC 3-1 JKT Tanzania (Alifungwa moja Ligi Kuu Uhuru)
    Simba SC 2-1 Mtibwa Sugar (Alifungwa moja Ligi Kuu Uhuru)
    Simba SC 3-0 Kagera Sugar (Hakufungwa Ligi Kuu Kaitaba)
    Simba SC 2-0 Biashara United (Hakufungwa Ligi Kuu Musoma)
    Simba SC 1-0 Mashujaa FC (Hakufungwa Kirafiki Kigoma)
    Simba SC 1-0 Azam FC (Hakufungwa Ligi Kuu Taifa)
    Simba SC 1-0 Singida United (Hakufungwa Ligi Kuu Arusha)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AISHI KUDAKA MECHI YA 100 LEO TANGU ASAJILIWE SIMBA JUNI 2017 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top