• HABARI MPYA

    Sunday, November 04, 2018

    SUAREZ AFUNGA DAKIKA YA MWISHO, BARCA YASHINDA UGENINI

    Luis Suarez akishangilia baada ya kufunga dakika ya 90 akimalizia pasi ya Sergi Roberto kuipatia Barcelona bao la ushindi ikiwalaza wenyeji, Rayo Vallecano 3-2 katika mchezo wa La Liga jana Uwanja wa Rayo Vallecano mjini Vallecas Teresa Rivero, Madrid. Hilo lilikuwa bao la pili Suarez kufunga jana, baada ya lingine dakika ya 11akimalizia pasi ya Jordi Alba, huku bao la lingine la Barca likifungwa na Ousmane Dembele dakika ya 87 na mabao ya Rayo Vallecano yalifungwa na Jose Angel Pozo dakika ya 35 na Alvaro Garcia dakika ya 57 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUAREZ AFUNGA DAKIKA YA MWISHO, BARCA YASHINDA UGENINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top