• HABARI MPYA

    Wednesday, November 28, 2018

    AGUERO AINUSURU MAN CITY KUCHAPWA NA LYON UFARANSA, SARE 2-2

    Sergio Aguero akinyoosha mkono juu kishujaa kufurahia bao la kusawazisha aliloifungia Manchester City dakika ya 83 ikipata sare ya 2-2 ugenini dhidi ya wenyeji, Lyon usiku wa jana kwenye mchezo wa Kundi F Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Groupama Stadium mjini Decines-Charpieu. Bao la kwanza lililokuwa la kusawazisha pia la Man City lilifungwa na Aymeric Laporte wakati mabao yote ya Lyon yamefungwa na Maxwel Cornet na yote kwa pasi za Memphis Depay dakika za 55 na 81.
    Kwa ushindi huo, Man City wanamaliza kileleni mwa Kundi F kutokana na pointi zao 10, wakifuatiwa na Lyon yenye pointi saba na zote zinakwenda hatua ya 16 Bora, zikizipiku Shakhtar Donetsk na Hoffenheim 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AGUERO AINUSURU MAN CITY KUCHAPWA NA LYON UFARANSA, SARE 2-2 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top