• HABARI MPYA

    Wednesday, November 28, 2018

    PETRONILA SIRINYA WA GOBA AWA MWANAMKE WA TATU TU KUSHINDA BAJAJI YA SHINDA ZAIDI NA SPORTPESA KATIKA DROOO YA 64

    TIMU Shinda Zaidi na SportPesa imebahatika kumpata mshindi mwigine mwanamama akiwa ni mwanamke wa tatu kujishindia Bajaji kutoka jiji la Dar es Salaam,Goba..
    Katika droo ya 64 Petronila Sirinya ambaye alibashiri na moja kwa moja kuingia kwenye droo ya Shinda Zaidi na SportPesa na kujishindia Bajaji Re kutoka SportPesa.
    Mshindi Huyo wa Droo ya 64 alisema alianza kushawishika kucheza na SportPesa baada ya kuona vile watu wengine wanashinda kwenye promosheni ya Shinda zaidi ndipo na yeye kuchukua uamuzi wa kuanza kucheza na timu ya kushinda kuutafuta ushindi wake.
    "Nimeufurahia ushindi huu sijawahi kushinda kabisa tena mimi ni mama wa nyumbani sikufikiri kama ningeshinda lakini Mungu kanisaidia sasa ntaweza kumudu mahitaji yangu kutoka kukaaa nyumbani mpaka kumiliki bajaji yangu hizi ni baraka kubwa sana kutoka kwenu SportPesa" alisema Petronila.
    Petronila Sirinya akikabidhiwa Bajaji yake baada ya kujishindia katika droo ya 64 ya Shinda Zaidi na SportPesa 
    Aidha Petronila alisema kipato atakachopata kupitia bajaj hiyo kitamsaidia kujiendeleza kielimu zaidi huku pesa nyingine ataziwekea mipango mizuri kumuwezesha mtoto kusoma shule nzuri.
    "Najua hata mume wangu atakuwa ameshawishika sasa maana wakati nacheza alikuwa ananiambia shauri yako unapoteza pesa zako lakini baada ya kushinda yeye ndio ananisisitiza niendelee kucheza kweli ushindi una raha yake " alisema Petronila Sirinya.
    Upande mwingine aliipongeza SportPesa kwa kutoa huduma bora kwa wateja wake sambamba na kuwajali kwa kuwatumia pesa za ushindi mara baada tu ya mechi kumalizia, huku akiweka wazi mikakati yake ya kuanza kusaka mtonyo wa Jackpot.
    Kutoka SportPesa, Meneja Uhusiano Bi. Sabrina H. Msuya alisema kampuni yetu inahuduma mbalimbali ambazo mteja akicheza anaweza kujishindia pesa ambazo anapata mara baada ya kuweka ubashiri wake na kupatia kiusahihi, Bajaji , Simu janja pamoja na Jezi orijino za Simba na Yanga.
    “Wikii hii Jackpot yetu imepanda mpaka shilingi 403,525,820/= ambapo mteja akibashiri kwa usahihi mechi kumi na tatu, na kuzawadiwa bonasi kwa watakao bashiri kwa usahihi kwa usahihi kuanzia mechi kumi hadi kumi na mbili.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PETRONILA SIRINYA WA GOBA AWA MWANAMKE WA TATU TU KUSHINDA BAJAJI YA SHINDA ZAIDI NA SPORTPESA KATIKA DROOO YA 64 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top