• HABARI MPYA

    Monday, November 06, 2017

    TAIFA STARS WALIVYOANZA MAZOEZI LEO GEREZANI KUJIANDAA NA BENIN

    Wachezaji wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wakifanya mazoezi leo Uwanja wa Kituo cha Michezo kwa Vijana cha Jakaya Kikwete (JKM Youth Centre), eneo la Gerezani, zamani Kidongo Chekundu, Dar es Salaam kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya wenyeji, Benin Novemba 11, mwaka huu 
    Mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajib akimpita winga wa Difaa Hassan El Jadida ya Morocco, Simon Msuva
    Yohana Oscar Nkomola (kulia) aliyepandishwa kutoka timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys akimiliki mpira  
    Wachezaji wakifanya mazoezi leo JKM Youth Centre
    Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga (wa pili kushoto) akijadiliana na wasaidizi wake, Patrick Mwangata na Fulgence Novatus (kulia) na Amy Ninje (kushoto). Taifa Stars inatarajiwa kuondoka nchini Alhamisi. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS WALIVYOANZA MAZOEZI LEO GEREZANI KUJIANDAA NA BENIN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top