• HABARI MPYA

    Friday, July 10, 2020

    MAN CITY NA JUVE AU LYON ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA

    TIMU ya Manchester City ikifuzu Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itakutana na Juventus au Lyon, wakati Chelsea itamenyana na ama Napoli au Barcelona kama watapindua matokeo dhidi ya Bayern Munich.
    City ipo kwenye nafasi nzuri ya kutinga Robo Fainali baada ya ushindi wa 2-1 dhidi Real Madrid kwenye mchezo wa kwanza wa Hatua ya 16 Bora Februari 26 Uwanja wa Bernabeu na zitarudiana Uwanja wa Etihad Agosti 7.
    Wakati huo huo, Chelsea wana mtihani mgumu kufuzu Robo Fainali baada ya kuchapwa 3-0 nyumbani na Bayern Munich Februari 25 na mechi ya marudiano itafuatia Ujerumani Agosti 7 pia. 
    Nao RB Leipzig baada ya kuitoa Tottenham katika 16 Bora itamenyana na Atletico Madrid, wakati Atalanta watamenyana na vigogo wa Ufaransa, Paris Saint-Germain na mechi hizo zitapigwa kati ya Agosti 12 na 15.

    RATBA KAMILI YA LIGI YA MABINGWA
    Robo Fanal
    Jumatano, Agosti 12: Atalanta vs PSG
    Alhamisi, Agosti 13: RB Leipzig vs Atletico Madrid
    Ijumaa, Agosti 14: Barcelona/Napoli vs Bayern Munich/Chelsea
    Jumamosi, Agosti 15: Manchester City/Real Madrid vs Juventus/Lyon 
    Nusu Fanal
    Jumanne, Agosti 18: Mshindi Robo-Fainali 2 vs Mshindi Robo-Fainali 1
    Jumatano, Agosti 19: Mshindi Robo-Fainali 4 vs Mshindi Robo-Fainali 3 
    Fainali 
    Jumapili, Agosti 23: 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY NA JUVE AU LYON ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top