• HABARI MPYA

    Sunday, August 18, 2019

    SIKU DEO NJOHOLE ‘OCD’ ALIPOTUA YANGA KAMA MCHEZAJI MWALIKWA

    WACHEZAJI wa Yanga SC kutoka kulia Lawrence Mwalusako, mchezaji mwalikwa kutoka Simba, Deo Njohole ‘OCD’, Abubakar Salum ‘Sure Boy’, Ramadhani Kilambo na Wastara Baribari aliyeipa mgongo kamera wakati wa mapumziko kwenye mchezo wa kirafiki mwaka 1991 dhidi ya timu ya taifa ya Uganda Uwanja wa Taifa (sasa Uhuru) mjini Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka 1-1, Njohole akiisawazishia Yanga baada ya The Cranes kutangulia kwa bao la Majid Musisi (sasa marehemu).  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIKU DEO NJOHOLE ‘OCD’ ALIPOTUA YANGA KAMA MCHEZAJI MWALIKWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top