Na Mwandishi Wetu, DODOMA
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limewaonya vikali viongozi na mashabiki wa klabu ya Yanga wanaopanga kuvuruga mchakato wa uchaguzi wa klabu hiyo.
Yanga wanatarajiwa kufanya uchaguzi wake Januari 13, mwakani kwa ajili ya kuziba nafasi zilizokuwa wazi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Malangwe Mchungahela, alisema TFF haitowavumilia wote watakaothubutu kuvuruga mchakato huo.
Mchungahela alisema kuwa wamebaini kwamba kuna mkakati wa baadhi ya viongozi wa kamati ya utendaji na mashabiki wa kutaka kuitisha mkutano kesho wenye lengo la kupinga uchaguzi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Malangwe Mchungahela amesema TFF haitowavumilia wanataka kuvuruga uchaguzi wa Yanga
“Taarifa zao tunazo, kwamba wanataka kuitisha kikao cha kupinga uchaguzi, hivyo sisi kama TFF tunawaonya wasithubutu, kwani tutawashughulikia kwa kutaka kuharibu mchakato huo na pia yeyote yule anayetaka uongozi asipite mlango wa nyuma, tukibaini hilo basi tutawashughulikia ikiwemo kuwapeleka kwenye kamati ya maadili,"amesema Mchungahela.
Mchungahela alisema kuwa awali walishakutana na viongozi waliobakia kwenye timu hiyo ambapo waliridhia kuendelea na mchakato wa uchaguzi hivyo kwa wanaotka kuharibu wanajitafutia matatizo.
Aidha Mchungahela alisema kuwa tayari fomu za uchaguzi zimeshaanza kutolewa tangu jana na mwisho wa kuchukua fomu hizo ni Desemba 14 mwaka huu.
Mbali na Manji viongozi wengine wa Yanga waliojiondoa ni Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji Hashim Abdala, Salum Mkemi na Omar Said.
Kufuatia hatua hiyo, Novemba mbili mwaka huu, Baraza la Michezo Taifa (BMT) kupitia kwa Kaimu Katibu Mkuu, Alex Kayenge iliitaka Yanga kufanya uchaguzi na kuitaka Kamati ya Uchaguzi ya TFF kusimamia uchaguzi huo ikiwemo bayana nafasi zinazopaswa kugombewa.
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limewaonya vikali viongozi na mashabiki wa klabu ya Yanga wanaopanga kuvuruga mchakato wa uchaguzi wa klabu hiyo.
Yanga wanatarajiwa kufanya uchaguzi wake Januari 13, mwakani kwa ajili ya kuziba nafasi zilizokuwa wazi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Malangwe Mchungahela, alisema TFF haitowavumilia wote watakaothubutu kuvuruga mchakato huo.
Mchungahela alisema kuwa wamebaini kwamba kuna mkakati wa baadhi ya viongozi wa kamati ya utendaji na mashabiki wa kutaka kuitisha mkutano kesho wenye lengo la kupinga uchaguzi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Malangwe Mchungahela amesema TFF haitowavumilia wanataka kuvuruga uchaguzi wa Yanga
“Taarifa zao tunazo, kwamba wanataka kuitisha kikao cha kupinga uchaguzi, hivyo sisi kama TFF tunawaonya wasithubutu, kwani tutawashughulikia kwa kutaka kuharibu mchakato huo na pia yeyote yule anayetaka uongozi asipite mlango wa nyuma, tukibaini hilo basi tutawashughulikia ikiwemo kuwapeleka kwenye kamati ya maadili,"amesema Mchungahela.
Mchungahela alisema kuwa awali walishakutana na viongozi waliobakia kwenye timu hiyo ambapo waliridhia kuendelea na mchakato wa uchaguzi hivyo kwa wanaotka kuharibu wanajitafutia matatizo.
Aidha Mchungahela alisema kuwa tayari fomu za uchaguzi zimeshaanza kutolewa tangu jana na mwisho wa kuchukua fomu hizo ni Desemba 14 mwaka huu.
Mbali na Manji viongozi wengine wa Yanga waliojiondoa ni Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji Hashim Abdala, Salum Mkemi na Omar Said.
Kufuatia hatua hiyo, Novemba mbili mwaka huu, Baraza la Michezo Taifa (BMT) kupitia kwa Kaimu Katibu Mkuu, Alex Kayenge iliitaka Yanga kufanya uchaguzi na kuitaka Kamati ya Uchaguzi ya TFF kusimamia uchaguzi huo ikiwemo bayana nafasi zinazopaswa kugombewa.
0 comments:
Post a Comment