• HABARI MPYA

    Friday, November 03, 2017

    MOURINHO AKUBALI KULIPA KODI ALIYOKWEPA HISPANIA PAUNI MILIONI 3

    KOCHA Jose Mourinho amekubali kuilipa Mamlaka ya Kodi ya Hispania kiasi cha Pauni Milioni 2.94 anazododaiwa kutolipa wakati alipokuwa anafundisha Real Madrid.
    Kocha huyo wa Manchester United aliwasili chumba namba nne cha mahakama ya Pozuelo de Alarcon, nje kidogo ya Jiji la Madrid Saa 3.33 asubuhi na shauri lake likasikilizwa Saa 4:00.
    Anatuhumiwa kukwepa kodi kati ya mwaka 2010 na 2013, lakini akawaambia Waandishi wa Habari nje ya mahakama baada ya shauri lake kusikilizwa kwamba hajakataa kulipa.
    Jose Mourinho amekubali kuilipa Mamlaka ya Kodi ya Hispania kiais cha Pauni Milioni 2.94 anazododaiwa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MOURINHO AKUBALI KULIPA KODI ALIYOKWEPA HISPANIA PAUNI MILIONI 3 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top