• HABARI MPYA

    Sunday, February 07, 2016

    AZAM FC YAREJEA NA MOTO LIGI KUU, YAITANDIKA 1-0 MWADUI...TOTO YAIPIGA 2-1 COASTAL

    MATOKEO LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
    Februari 7, 2016
    Kagera Sugar 0-1 Simba SC
    Mbeya City 0-0 Prisons
    JKT Ruvu 0-4 Yanga SC
    Ndanda FC 1-1 Mtibwa Sugar
    Azam FC 1-0 Mwadui FC
    Toto Africans 2-1 Coastal Union
    Majimaji 1-0 Mgambo JKT
    Februari 6, 2016
    African Sports 0-0 Stand United
    Kipre Tchetche ameing'arisha Azam FC leo

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    BAO pekee la mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche limaipa Azam FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Mwadui FC jioni ya leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Kipre Tchetche, mchezaji wa zamani wa timu ya vijana ya Ivory Coast, alifunga bao hilo dakika ya 18 akimalizia pasi ya Nahodha John Bocco.
    Na kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 42 baada ya kucheza mechi 16, ikizidiwa pointi moja na mabingwa watetezi, Yanga SC waliocheza mechi mbili zaidi.
    Azam FC sasa inafungana kwa pointi na Simba SC, inayokaa nafasi ya pili kwa wastani wake mzuri wa mabao, ingawa na wao wamecheza mechi mbili zaidi. 
    Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Simba SC imeshinda 1-0 dhidi ya Kagera Sugar Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Yanga SC imeshinda 4-0 dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Mbeya City imetoka sare ya 0-0 na Prisons Uwanja wa Sokoine, Mbeya. 
    Ndanda FC imelazimishwa sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, Toto Africans imeshinda 2-1 dhidi ya Coastal Union Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Majimaji imeshinda 1-0 dhidi ya Mgambo JKT Uwanja wa Majimaji, Songea, wakati jana African Sports ilitoa sare ya 0-0 na Stand United Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
    Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Erasto Nyoni, David Mwantika, Serge Wawa, Jean Mugiraneza, Himid Mao/Kipre Balou dk70, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Frank Domayo dk78, Ramadhani Singano ‘Messi’, Kipre Tchetche/Allan Wanga dk66na John Bocco.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAREJEA NA MOTO LIGI KUU, YAITANDIKA 1-0 MWADUI...TOTO YAIPIGA 2-1 COASTAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top