• HABARI MPYA

    Saturday, February 20, 2016

    NGASSA AGONGA ZOTE 90 FREE STATE YACHAPWA 2-0 UGENINI LIGI KUU AFRIKA KUSINI

    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa (pichani juu) amecheza dakika zote 90 timu yake, Free State Stars ikichapwa mabao 2-0 na Chippa United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Absa Afruka Kusini Uwanja wa Nelson Mandela Bay mjini Port Elizabeth leo.
    'Chilli Boys' wanabaki nafasi ya sita katika msimamo wa ligi pamoja na ushindi huo, huku Ea Lla Koto wakiporomoka hadi nafasi ya nane.
    Mabao ya Chippa yamefungwa na Xola Mlambo dakika tatu kabla ya mapumziko na Nkosinathi Mthiyane dakika ya 72.

    Kikosi cha Chippa kilikuwa: Akpeyi, Mthiyane/Zuke dk90, Okwuosa, Macheke, Thopola, Chipeta, Mlambo, Sangweni, Bance/R. Manzini dk65, Zulu/Sali dk43 na Molangoane.
    Free State Stars: Diakite, Masehe, Mashego, Sankara/Venter dk74, Chabalala, Kerspuy, Thebakang/Gopane dk11, Jaftha/Nkosi dk45, Thethani, Ngassa na Vilakazi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NGASSA AGONGA ZOTE 90 FREE STATE YACHAPWA 2-0 UGENINI LIGI KUU AFRIKA KUSINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top