• HABARI MPYA

    Sunday, December 20, 2015

    AZAM FC YAITANDIKA MAJIMAJI 2-1, MBEYA CITY ‘ULIMI NJE’ KWA MGAMBO SOKOINE

    RATIBA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
    Leo; Desemba 20, 2015
    Majimaji 1-2 Azam FC
    JKT Ruvu 2-2 Coastal Union
    Mbeya City 1-1 Mgambo JKT
    Jana; Desemba 19, 2015
    Yanga SC 4-0 Stand United
    Mwadui FC 2-1 Ndanda FC
    Kagera Sugar 1-0 African Sports
    Prisons 0-0 Mtibwa Sugar
    Toto Africans 1-1 Simba SC
    MECHI ZIJAZO…
    Desemba 23, 2015
    Azam FC vs Mtibwa Sugar
    Desemba 26, 2015
    Ndanda FC vs JKT Ruvu
    Yanga SC vs Mbeya City
    Majimaji vs Prisons
    Mwadui FC vs Simba SC
    Mtibwa Sugar vs Mgambo JKT
    Coastal Union vs Stand United
    Desemba 27, 2015
    Azam FC vs Kagera Sugar
    Toto Africans vs African Sports
    Didier Kavumbangu ameifungia Azam FC leo ikishinda 2-1 ugenini

    AZAM FC imepata ushindi muhimu wa ugenini, baada ya kuifunga mabao 2-1 Majimaji Uwanja wa Majimaji Songea jioni ya leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
    Ushindi huo unaifanya Azam FC ifikishe pointi 29 baada ya kucheza mechi 11 na kuendelea kubaki nafasi ya pili, nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 30 na mechi moja zaidi.  
    Mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC, Didier Kavumbangu alianza kuifungia Azam FC dakika ya 10, kabla ya Ame Ally ‘Zungu’ kufunga la pili dakika ya 20.
    Bao pekee la wenyeji, Majimaji lilifungwa na Alex Kondo dakika ya 55.
    Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Serge Wawa, David Mwantika, Farid Mussa, Frank Domayo, Jean Mugiraneza, Ame Ally/Allan Wanga dk85, John Bocco na Didier Kavumbagu.
    Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, JKT Ruvu imelazimishwa sare ya 2-2 na Coastal Union Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, wakati Mbeya City nayo imelazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo JKT Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAITANDIKA MAJIMAJI 2-1, MBEYA CITY ‘ULIMI NJE’ KWA MGAMBO SOKOINE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top