• HABARI MPYA

    Saturday, August 30, 2014

    STRAIKA LA MAN UNITED LAIKALISHA MAN CITY ETIHAD

    MABINGWA watetezi, Manchester City wamepunguzwa kasi katika Ligi Kuu ya England baada ya kupata kipigo cha kwanza msimu huu mbele ya Stoke City 1-0 Uwanja wa Etihad leo.
    Alikuwa ni Mame Biram Diouf aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 58, baada ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United kuwatoka mabeki wa City na kumaliza uteja wa kufungwa mechi sita mfululizo Etihad.
    Kikosi cha Man City kilikuwa; Hart, Sagna, Kompany, Demichelis, Kolarov, Silva, Fernando/Fernandinho dk38, Toure, Nasri/Navas dk63, Jovetic/Dzeko dk63 na Aguero. 
    Stoke: Begovic, Bardsley, Shawcross, Wilson, Pieters, Walters/Odemwingie dk45, Adam, Whelan, Nzonzi, Moses/Muniesa dk80, Crouch na Diouf. 
    Diouf akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Stoke City Uwanja wa Etihad
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: STRAIKA LA MAN UNITED LAIKALISHA MAN CITY ETIHAD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top