Hiki ndicho kikosi cha kwanza cha Simba SC, ambacho kocha Patrick Phiri amekuwa akikitanguliza dakika 45 za kwanza katika mechi zake visiwani Zanzibar. Na hiki ndicho kikosi kilichomaliza kipindi cha kwanza kinaongoza 4-0 dhidi ya KMKM jana katika ushindi wa 5-0. Kutoka kulia waliosimama ni Joram Mgeveke, Miraj Adam, Ivo Mapunda, Joseph Owino, Amri Kiemba, na Haroun Chanongo. Waliochuchumaa kutoka kulia ni Ramadhani Singano 'Messi', Pierre Kwizera, Shaaban Kisiga, Amisi Tambwe na Issa Rashid. Wachezaji watatu wa kiwango cha juu, Emmanuel Okwi, Paul Kiongerea na Jonas Mkude hawapo hapa. Na kuna wachezaji wa kikosi cha pili kama Said Ndemla, Elias Maguri, Twaha Ibrahim 'Messi' wanafanya vizuri. Hii inamaanisha Simba SC ipo vizuri kuelekea msimu ujao. |
0 comments:
Post a Comment