• HABARI MPYA

    Thursday, August 28, 2014

    RAIS TFF KUZURU MANYARA, KILIMANJARO, ARUSHA

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atatembelea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
    Katika ziara hiyo atakutana na viongozi na kuangalia hali hali ya mpira wa miguu katika mikoa hiyo na mahitaji yake. Pia atazungumzia maono (vision) ya TFF katika mpira wa miguu.
    Rais Malinzi atawasili mkoani Manyara, Agosti 29 mwaka huu, na ataanza ziara rasmi katika mkoa huo Agosti 30 mwaka huu. Agosti 31 mwaka huu atakuwa Arusha, na kumalizia Septemba 1 mkoani Kilimanjaro.
    Rais wa TFF, Jamal Malinzi

    Katika ziara hiyo, Rais Malinzi atafuatana na Mkurugenzi Msaidizi (Wanachama) wa TFF, Eliud Mvella. Pia Septemba 8 mwaka huu, Rais Malinzi ataanza ziara ya mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RAIS TFF KUZURU MANYARA, KILIMANJARO, ARUSHA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top