• HABARI MPYA

    Friday, July 11, 2014

    RONALDO ANAVYOJIFARIJI KWA 'MISTAREHE' BAADA YA KUTOLEWA KOMBE LA DUNIA...MESSI ANAPETA BRAZIL

    NYOTA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo anaendelea kujifariji baada ya kutolewa Kombe la Dunia kwa kula raha na mpenzi wake, Irina Shayk.
    Akiwa ameshindwa kuisaidia Ureno iliyotolewa hatua ya makundi Kombe la Dunia nchini Brazil, ameposti picha akiwa na mpenzi wake Irina Shayk wake nje ya helikopta asubuhi ya leo wanajiandaa kupanda chombo hicho kwenda kwenye matanuzi.
    Ronaldo ambaye wiki iliyopita aliposti picha akiwa na Irina, leo ameposti picha hiyo akiwa nje ya helikpota akiambatanisha na ujumbe usemao; 'safari asubuhi'.

    Kupaa juu: Cristiano Ronaldo akiwa na mpenzi wake, Irina Shayk tayari kwa safari yao ya asubuhi
    Posers: Cristiano Ronaldo (left) pictured in a selfie with Russian model girlfriend Irina Shayk (right)
    Mapozi: Cristiano Ronaldo (kushoto) awali aliposti picha hii akiwa na 'mupenz', mwanamtindo wa Urusi, Irina Shayk kulia

    Wakati Mwanasoka huyo Bora wa Dunia anakula bata, mpinzani wake mkubwa, nyota wa Barcelona, Lieonel Messi anaendelea kutesa uwanjani akiwa ameiwezesha Argentina kutinga Fainali Kombe la Dunia, baada ya kuitoa Uholanzi kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 120.
    Sasa Messi anaingia kwenye jaribio la kutwaa Kombe la kwanza la Dunia atakapoiongoza Argentina katika Fainali Jumapili dhidi ya Ujerumani. 
    Date with destiny: Lionel Messi is one game away from leading Argentina to World Cup glory
    Mambo uwanjani: Lionel Messi anaendelea kutesa katika Kombe la Dunia, wakati Ronaldo anajifariji kwa starehe
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO ANAVYOJIFARIJI KWA 'MISTAREHE' BAADA YA KUTOLEWA KOMBE LA DUNIA...MESSI ANAPETA BRAZIL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top