• HABARI MPYA

    Thursday, July 24, 2014

    VAN GAAL AANZA NA 7-0 MAN UNITED

    KOCHA Louis van Gaal ameanza vizuri Manchester United baada ya kuiongoza kushinda mabao 7-0 katika mchezo wa kirafiki dhidi ya wenyeji LA Galaxy nchini Uwanja wa Rose Bowl Pasadena.
    Huu ndiyo Uwanja ambao ulitumika kwa Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1994 na United ikicheza mechi ya kwanza chini ya Van Gaal ilikonga nyoyo za mashabiki wake kwa soka safi.
    Mabao ya Man United yamefungwa na Welbeck dakika ya 13, Wayne Rooney dakika za 41 kwa penalti na 45, James dakika za 62 na 84 na Young dakika za 88 na 90.
    Safi kijana: Mshambuliaji wa Man United, Rooney akimpongeza mwenzake, Danny Welbeck baada ya kufunga bao la kwanza
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAN GAAL AANZA NA 7-0 MAN UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top