• HABARI MPYA

    Sunday, June 29, 2014

    AVEVA ASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI SIMBA SC

    Matokeo ya awali ambayo BIN ZUBEIRY imeyapata kutoka chumba cha kuhesabia kura ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam, Evans Elieza Aveva ameshinda Urais kwa kupata kura 1452 kati ya 1845 zillizopigwa, mpinzani wake Andrew Tupa akipata kura 387 wakati kura sita zimeharibika. Hata hivyo, matokeo rasmi ya uchaguzi huo yatatangazwa na Kamati ya Uchaguzi ya klabu hiyo chini ya Mwenyekiti Dk Damas Ndumbaro baadaye.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AVEVA ASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top