• HABARI MPYA

    Friday, June 27, 2014

    16 BORA KOMBE LA DUNIA HII HAPA, NIGERIA NA UFARANSA, ALGERIA NA UJERUMANI...BRAZIL NA CHILE

    TIMU za Afrika zilizofuzu 16 Bora ya Kombe la Dunia nchini Brazil zitakutana na mabingwa wa zamani wa michuano hiyo katika hatua hiyo.
    Nigeria itamenyana na Ufaransa wakati Algeria itamenyana na Ujerumani- kuwania kuungana na Cameroon, Senegal na Ghana katika orodha ya timu za Afrika zilizowahi kufika Robo Fainali ya Kombe la Dunia.
    Mechi nyingine za Robo Fainali ni kati ya Brazil na Chile, Colombia na Uruguay, Uholanzi na Mexico, Argentina na Uswisi na Ubelgiji na Marekani.
    Kitu hicho: Islam Slimani wa Algeria akimtungua kipa wa Urusi, Igor Akinfeev kuifungia timu yake bao katika sare ya 1-1 usikua wa kuamkia leo, ambao inaipeleka timu hiyo ya Afrika hatua ya mtoano ya Kombe la Dunia, ambako itamenyana na Ujerumani
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: 16 BORA KOMBE LA DUNIA HII HAPA, NIGERIA NA UFARANSA, ALGERIA NA UJERUMANI...BRAZIL NA CHILE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top