• HABARI MPYA

    Monday, December 17, 2018

    MAN UNITED YAPEWA PSG 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA

    TIMU ya Manchester United itamenyana na Paris Saint-Germain katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
    Timu nyingine tatu za England nazo zimepangiwa wapinzani wagumu kutoka Ujerumani katika hatua hiyo.
    Liverpool imepangiwa Bayern Munich, wakati Manchester City itamenyana na Schalke na Tottenham Hotspur imepewa Borussia Dortmund.
    Kikosi cha Jose Mourinho kinachosuasua kitaanzi nyumbani Uwanja wa Old Trafford kabla ya kusafiri kuwafuata matajiri wa Ufaransa kwa mchezo wa marudiano.


    RATIBA KAMILI HATUA YA 16 BORA YA LIGI YA MABINGWA UKAYA

    Schalke vs Manchester City
    Atletico Madrid vs Juventus
    Manchester United vs PSG
    Tottenham vs Borussia Dortmund 
    Lyon vs Barcelona
    Roma vs Porto 
    Ajax vs Real Madrid
    Liverpool vs Bayern 

    Man City, timu pekee ya England iliyoongoza kundi, itaanzia ugenini kabla ya kucheza nyumbani mechi ya marudiano, lakini timu nyingine zitaanzia ugenini.
    Mechi za kwanza zitachezwa Februari 12, 13, 19 na 20 na za marudiano zitachezwa Machi 5, 6, 12 na 13 mwaka 2019.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YAPEWA PSG 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top