• HABARI MPYA

    Sunday, October 28, 2018

    TANZANIA YAPANGWA KUNDI MOJA NA SENEGAL, NIGERIA NA LIBYA FAINALI ZA AFRIKA SOKA LA UFUKWENI

    Na Mwandishi Wetu, CAIRO
    TANZANIA imepangwa Kundi katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Soka la Ufukweni (Beach Soccer) zinazotarajiwa kuanza Desemba 8 hadi 14 mwaka huu nchini Misri.
    Katika droo iliyofanyika leo nchini Misri, Tanzania imepangwa kundi moja na Senegal, Nigeria na Libya, wakati Kundi A likiwa na timu za Misri, Morocco, Ivory Coast na Madagascar.
    Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufuzu fainali hizo tangu ianzishe timu ya soka la ufukweni na imefuzu baada ya Afrika Kusini kujitoa kwenye safari ya kusaka tiketi hiyo.

    Mechi zote za michuano hiyo inayoanza kujipatia umaarufu mkubwa barani Afrika zitafanyika mjini Sharm El Sheikh nchini Misri.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA YAPANGWA KUNDI MOJA NA SENEGAL, NIGERIA NA LIBYA FAINALI ZA AFRIKA SOKA LA UFUKWENI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top