• HABARI MPYA

    Monday, October 29, 2018

    HIDAYA JUMA WA DAR AWA MWANAMKE WA PILI KUJISHINDIA BAJAJI YA SPORTPESA

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    TIMU ya ushindi SportPesa inaendelea kufurahia mafanikio ya ushindi wa wateja wake hasa baada ya washindi wengi wa bajaji kutoa simulizi zinazoonyesha kuwa maisha yao yanaenda kubadilika baada ya kushinda.
    Na wakati huu ni zamu nyingine ya mshindi wa Shinda Zaidi Na SportPesa, Hidaya Juma wa hapa Jijini Dar es Salaam kukabidhiwa bajaji yake baada ya kushinda.
    huyu anakuwa mwanamke wa pili kuondoka na bajaji kwenye promosheni hii na yeye hakuwa nyuma kutuelezea siri ya ushindi wake ambapo alisema kuwa mume wake ndio alimuelekeza kucheza na SportPesa mpaka kushinda.
    "Mimi nimeshinda na nafurahia kwa zawadi hii kutoka SportPesa unajua hapo mwanzo nilidhani labda mchezo huu ni wanaume lakini nivyoona mpaka kina mama wanashinda ndipo nilipomuomba mume wangu anielekeze maana na yeye alikuwa tayari anacheza na sportpesa na mara baada ya kunifundisha na mimi kuanza haikunichukua muda hadi siku napigiwa simu kuwa nimeshinda bajaj kweli nashukuru sana " alisema Hidaya 
    Hidaya Juma wa Dar es Salaam akionyesha funguo ya bajaji aliyokabidhiwa na Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa, Tarimba Abbas (kulia)
    Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa, Tarimba Abbas (kulia) akimkabidhi zawadi zake, Hidaya Juma (katikati) mjini Dar es Salaam

    Kwa upande mwingine mshindi huyo aliwataka wakinamama wenzake kuichangamkia fursa hii kutoka SportPesa huku akiwaeleza kuwa hii inaweza kuwa sehemu muhimu kwao kujikwamua kuichumi na kuongeza kipato kuliko kutegemea kukaa nyumbani na kubaki kuwa tegemezi.
    Akimkabidhi bajaji Hiyo Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti Kutoka SportPesa Tarimba Abbas alimpongenza mwanamama huyo kwa juhudi zake za kupambana kucheza na SportPesa mpaka kufanikiwa kushinda bajaj.
    "huu ni mfano mzuri kwa wakinamama wote na watanzania kwa ujumla kuwa mambo haya yanawezekana muhimu ni kujisajisajili ya SportPesa na kuanza kucheza kwa sababu huwezi kujua bahati yako unaweza kuala maskini lakini kesho ukaamka na utajiri kutoka SportPesa nawaomba mcheze sana maana bajaj Bado zipo" alisema Tarimba 
    Huu ni muendelezo wa SportPesa kutoa zawadi mbalimbali kwa washindi wanaocheza na kampuni hiyo pendwa ya ubashiri hapa nchini na kila siku mshindi mmoja hukabidhiwa bajaj unachotakiwa kufanya ni kupiga *150*87# au kucheza kwa tovuti yani www.sportpesa.co.tz
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HIDAYA JUMA WA DAR AWA MWANAMKE WA PILI KUJISHINDIA BAJAJI YA SPORTPESA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top