• HABARI MPYA

    Friday, November 03, 2017

    SIMBA QUEENS KUFUNGUA DIMBA NA FAIR PLAY LIGI YA WANAWAKE

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    TIMU ya soka ya Simba Queens itafungua dimba na Fair Play ya Tanga katika Ligi Kuu ya Taifa ya Wanawake Tanzania Bara Novemba 27, mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
    Simba imepangwa Kundi A katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Novemba 26, mwaka huu chini ya udhamini wa Azam TV.
    Simba imepangwa Kundi A mbalo mechi zake zitafanyika katika Kituo cha Dar es Salaam Uwanja wa Karume. Katika kundi hilo, Simba Queens iliyopanda daraja msimu huu ipo pamoja mabingwa watetezi, Mlandizi Queens, Mburahati Queens, JKT Queens, Evergreen zote za Dar es Salaam na Fair Play ya Tanga.
    Kundi B litakuwa na timu za Alliance ya Mwanza ambayo imepanda kutoka kituo cha Dodoma. Timu nyingine ni Marsh Academy pia ya Mwanza; Panama ya Iringa; Kigoma Sisterz ya Kigoma, Baobab ya Dodoma na Majengo Queens ya Singida.
    Fungua dimba kwa Kituo cha Dar es Salaam, mabingwa watetezi wa taji hilo, Mlandizi Queens itacheza na JKT Queens katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.
    Katika kundi hilo la A, mechi nyingine zitakuwa siku inayofuata Novemba 27, mwaka huu kati ya Mburahati Queens na Evergreen saaa 8.00 mchana wakati Fair Play ya Tanga itacheza na Simba Queens saa 10.00 jioni.
    Jijini Arusha, Panama ya Iringa itafungua dimba na Alliance Queens ya Mwanza huku siku ya pili Novemba 27, mwaka huu Baobab Queens itacheza na Marsh Academy saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni Majengo Queens itapambana na Sisterz ya Kigoma.
    Timu hizo zitapambana katika vituo hadi Desemba 12, mwaka huu kabla ya kutoa jumla ya timu nane kwa maana ya nne kutoka kila kundi. Timu hizo nane zitapambana katika hatua ya Nane Bora ya Ligi hiyo kuelekea ubingwa. Ligi inatarajiwa kumalizika Machi 28, mwakani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA QUEENS KUFUNGUA DIMBA NA FAIR PLAY LIGI YA WANAWAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top