• HABARI MPYA

    Sunday, September 27, 2015

    MESSI AUMIA BARCA IKISHINDA 2-1, RONALDO ASHINDWA KUIBEBA REAL

    TIMU ya Barcelona imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Hispania, La Liga kufuatia ushindi wa 2-1dhidi ya Las Palmas Jumamosi Uwanja wa Nou Camp.
    Katika mchezo huo, Barca ilipata pigo baada ya nyota wake, Lionel Messi kuumia dakika ya 10 na kushindwa kuendelea na baadaye ikagundulika anatakiwa kuwa nje kwa wiki nane.
    Mabao yote ya Barca yamefungwa na mshambuliaji wa zamani Liverpool, Luis Suarez, wakati bao la Palmas limefungwa na Viera Ramos huku Mbrazil, Neymar akipaisha penalti.
    Mchezo mwingine wa La Liga, Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo alishindwa kuisaidia Real Madrid baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Malaga Uwanja wa Bernabeu.
    Luis Suarez akiruka hewani kushangilia baada ya kuifungia Barcelona ikishinda 2-1 dhidi ya Las Palmas Uwanja wa Nou Camp  PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    The Santiago Bernabeu looked a lonely place for Ronaldo after he missed 13 attempts to score
    Ronaldo akiwa taabani Uwanja wa Santiago Bernabeu baada ya Real Madrid kulazimishwa sare ya 0-0 na Malaga PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AUMIA BARCA IKISHINDA 2-1, RONALDO ASHINDWA KUIBEBA REAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top