• HABARI MPYA

    Thursday, July 10, 2014

    SIMBA SC YAFANYA KUFURU, YASAINI WATATU KWA MPIGO LEO AKIWEMO MANYIKA JR. NA BEKI LA MWADUI

    Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
    SIMBA SC imesajili wachezaji wawili chupukizi kwa ajili ya timu yake ya vijana chini ya umri wa miaka 20, maarufu kama Simba B, akiwemo Peter Manyika, mtoto wa kipa wa zamani wa Yanga SC, Manyika Opeter. 
    Makamu Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesimamia zoezi hilo lililokamilika vyema akishirikiana na Mjumbe wa Kamati ya Usajili, Said Tuliy leo mjini Dar es Salaam.
    Said Tuliy kulia, Kaburu kushoto na Manyika Jr. katikati akisaini Simba SC

    Pamoja na kipa huyo wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Wekundu hao wa Msimbazi pia wamemsajili kinda mwingine kutoka Mwadui ya Shinyanga, kiungo mshambuliaji Ibrahim Hajibu Migomba, ambaye alipelekwa kwa mkopo huko msimu uliopita kutoka Simba B.
    Kaburu maarufu kama Perez, amesema mtoto wa Manyika amesaini miaka mitatu sawa na Hajibu ambao wote pamoja na kusajiliwa kama wachezaji wa Simba B, watakuwa wanakomazwa kikosi cha kwanza.
    Awali ya hapo, leo Simba SC ilimsajili kipa wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Hussein Sharrif ‘Cassilas’ aliyesaini Mkataba wa miaka miwili.
    Kaburu kushoto akiwa na Hajibu baada ya kusaini

    Kipa huyo bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara amekuwa akiibeba Mtibwa Sugar kwa misimu mitatu iliyopita, tangu kuondoka kwa Shaaban Hassan Kado.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC YAFANYA KUFURU, YASAINI WATATU KWA MPIGO LEO AKIWEMO MANYIKA JR. NA BEKI LA MWADUI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top