• HABARI MPYA

    Wednesday, July 09, 2014

    LIGI KUU BARA YASOGEZWA HADI SEPTEMBA 20 KUISUBIRI YANGA SC IRUDI KOMBE LA KAGAME

    Na Boniface Wambura, DAR ES SALAAM
    LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, msimu wa 2014/2015 itaanza kutimua vumbi Septemba 20 mwaka huu.
    Awali michuano hiyo ilikuwa ianze Agosti 24 mwaka huu, lakini Shirikisho la Soka Tanzania limelazimika kuisogeza mbele kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupitisha michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame).
    Michuano ya Kombe la Kagame inayoshirikisha mabingwa wa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) itafanyika Agosti mwaka huu nchini Rwanda.
    Yanga SC watashiriki Kombe la Kagame Rwanda 

    Timu 14 zitashiriki Ligi Kuu msimu huu. Timu hizo ni mabingwa watetezi Azam, Coastal Union, JKT Ruvu Stars, Kagera Sugar, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Ndanda FC, Polisi Morogoro, Ruvu Shooting, Simba, Stand United, Tanzania Prisons na Yanga.
    Ratiba ya ligi hiyo itatolewa mwezi mmoja kabla ya michuano hiyo kuanza kutimua vumbi. Yanga SC itaiwakilisha Tanzania kwenye Kombe la Kagame.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIGI KUU BARA YASOGEZWA HADI SEPTEMBA 20 KUISUBIRI YANGA SC IRUDI KOMBE LA KAGAME Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top