KIUNGO Gareth Barry ameondolewa kwenye kikosi cha timu ya
taifa kwa ajili ya Euro 2012, kwa sababu ya majeruhi ya nyonga, Chama cha Soka
kimethibitisha.
Kiungo huyo England mwenye umri wa miaka 31, alifanyiwa
vipimo mapema leo, ambavyo vimethibitisha ana maumivu makubwa.
"Ninasikitishwa sana kumpoteza Gareth," alisema
kocha Roy Hodgson. "Nina uhakika ataendelea kuwa sehemu ya kikosi cha
England baada ya Euros."
Hodgson amemuita beki wa Everton, Phil Jagielka kuchukua
nafasi ya Barry.
"Kikosi cha mwisho cha England cha wachezaji watatu
lazima iwe kimewasilishwa kwa ajili ya fainali hizo za Poland na Ukraine mchana
wa kesho.
Barry, ambaye ameichezea tmu ya taifa mechi 50, alilazimika
kutoka nje baada ya dakika 30 tu baada ya kuingia akitokea benchi katika mechi
ya kirafiki na Norway mjini Oslo, Jumamosi.
Uamuzi wa Hodgson kumuita Jagielka unaweza kumfanya Phil
Jones ahamie kwenye nafasi ya kiungo, ambako aliwahi kucheza wakati katika
klabu yake, Manchester United mwishoni mwa msimu.
Bado wachezaji Danny Welbeck na Glen Johnson, ambao wamepona
hivi karibuni maumivu ya kifundo cha mguu wanaangaliwa afya zao, na wawili hao
wanatarajiwa kuwasili kambini, Watford kesho.
Scott Parker pia alikuwa majeruhi, lakini amethibitisha yuko
fiti akitokea benchi dakika ya 55 katika mechi ya ushindi wa England wa 1-0
dhidi ya Norway mwishoni mwa wiki.
So könnten sie spielen
-
Im Achtelfinal-Rückspiel der UEFA Champions League tritt Borussia Dortmund
gegen den FC Sevilla an. Anstoß ist am Dienstag um 21.00 Uhr. Hier finden
Sie di...
Guber election. Bauchi students endorse pate
-
Paul Orude, Bauchi Coalition of Bauchi State Students and Youths Movement
has endorsed Dr Muhammad Ali Pate of the People’s Democratic Party (PDP)
for ...
YANGA ‘KUPAA’ JUMANNE KUIFUATA MWADUI FC
-
MARA baada ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc kwenye uwanja wa
Majaliwa, Lindi, siku ya jumapili, Kikosi cha Young Africans Sports Club,
kitareje...
0 comments:
Post a Comment