• HABARI MPYA

    Thursday, May 31, 2012

    TETESI ZA USAJILI BARA: MTIBWA, COASTAL ZAMGOMBEA KIUNGO FUNDI WA AZAM


    KIUNGO wa Azam FC aliyecheza kwa mkopo msimu huu, African Lyon ya Dar es Salaam, Suleiman Kassim ‘Selembe’ amesema kwamba Coastal Union ya Tanga na Mtibwa Sugar ya Morogoro, ndizo ambazo hadi sasa zimeonyesha nia ya kumsajili, ila anapenda kukabiliana na changamoto kubwa zaidi, kama za Simba au Yanga.
    Akizungumza na BIN ZUBEIRY visiwani Zanzibar leo asubuhi, Selembe (pichani kushoto) alisema kwamba klabu yake, Azam FC imeonyesha nia ya kumuacha aende klabu yoyote itakayomtaka na sasa naye anasikilizia timu ambayo itamalizana naye.
    “Kwa kweli hadi sasa naweza kusema Coastal Union na Mtibwa ndizo ambazo zimeonyesha nia haswa ya kunisajili, ila mimi mwenyewe niko tayari kukabiliana na changamoto zozote, hasa zile kubwa kubwa, kama Simba au Yanga hivi, niko tayari,”alisema.
    Selembe ni kati ya viungo wazuri kwa sasa nchini, ambaye ameyumba kidogo baada ya Azam kumpeleka kwa mkopo Lyon, kiasi cha kufikia kutemwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.
    Kwa sasa, fundi huyo wa soka yuko kwenye kambi ya timu ya Zanzibar, inayojiandaa na michuano ya Kombe la Dunia ya nchi zisizo wanachama wa FIFA nchini Uzbekistan, michuano itakayoanza Juni 4, mwaka huu na Zanzibar Heroes inatarajiwa kuondoka Juni 2 nchini.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TETESI ZA USAJILI BARA: MTIBWA, COASTAL ZAMGOMBEA KIUNGO FUNDI WA AZAM Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top