• HABARI MPYA

    Wednesday, May 23, 2012

    MTUKUTU BARTON ATUPWA JELA MECHI 12


    EPL: Carlos Tevez - Joey Barton, Manchester City v QPR
    Barton kulia akizunguana na Tevez anayeamuliwa na wachezaji wenzake wa Man City

    Getty

    NAHODHA wa QPR, Joey Barton amefungiwa mechi 12 na Chama cha Soka England kwa vurugu alizofanya kwenye mechi dhidi ya Manchester City katika siku ya mwisho ya msimu huu wa Ligi Kuu.
    Barton ameongezewa adhabu ya mechi nane katika mechi nne za awali sambamba na kutozwa faini ya pauni 75,000.
    Aligombana na Sergio Aguero na Vincent Kompany, lakini baada ya kupewa kadi nyekundu akamuanzishia na Carlos Tevez, na baadaye akawazingua marefa.
    Pamoja na hayo hajaadhibiwa kwa kwa kumsukumia kichwa Kompany, Tume Kanuni imesema katika taarifa kwa kitendo alichomfanyia Sergio Aguero anastahili adhabu hiyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTUKUTU BARTON ATUPWA JELA MECHI 12 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top