• HABARI MPYA

    Tuesday, May 29, 2012

    ALIYEFUKUZWA TWANGA PEPETA ATUA KIFALME MASHUJAA BAND

    Chaz Baba kulia akimwambia Martine karibu sana. Kushoto ni King Dodo La Bouche, mwasisi wa Mashujaa Band


    Martine katikaqti, King Dodoo kulia na Chaz Baba kushoto katika utambulisho wa Meneja huyo mpya asubuhi hii

    MENEJA aliyefukuzwa bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, Martine Sospeter leo ametangazwa rasmi kuwa Meneja mpya wa bendi ya Mashujaa- ikiwa ni siku mbili tu afukuzwe katika bendi yake ya awali iliyompatia umaarufu.
    Martine, ametambulishwa asubuhi hii katika mgahawa wa Business Park, Victoria, Dar es Salaam. Pamoja na utambulisho huo, Martine amekanusha madai ya Mkurugenzi wa Twanga Pepeta, Asha Baraka kwamba ametoweka na fedha za bendi hiyo.
    Katika taarifa yake ya kumfukuza kazi Martine, Asha alidai Meneja huyo alichukua fedha kwa wateja kwa ajili kuwakodisha bendi- hivyo akamtaka azirejeshe. “Sijachukua fedha yoyote popote, sina deni, kama anadai nina deni, alete ushahidi,”alisema Martine.
    Martine alisema kwamba kwa muda mrefu amekuwa akitakiwa na bendi ya Mashujaa kwa dau zuri, lakini amekuwa akikataa kutokana na jinsi anavyomheshimu Asha Baraka, lakini anasikitika amefukuzwa kwa kudhalilishwa.
    “Amenikfukuza na kunitolea maneno ya kashfa mimi wakati nipo na bendi yake ziarani mikoani, imeniuma sana. Ila bado nitaendelea kumuheshimu Asha Baraka kama dada yangu na mtu ambaye amenifikisha hapa.”alisema Martine.
    Sababu kubwa aliyoitaja Asha ya kumfukuza Martine ni kuwarubuni wanamuziki wa Twanga Pepeta kuhamia kwa wapinzani, Mashujaa. Miongoni mwa wanamuziki wa Twanga waliohamia Mashujaa ni mwimbaji hodari, Charles Baba.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ALIYEFUKUZWA TWANGA PEPETA ATUA KIFALME MASHUJAA BAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top