Hayo ni maneno ya beki wa zamani Liverpool, Mark Lawrenson

BEKI wa zamani wa Liverpool, Mark Lawrenson anaamini kuajiriwa kwa kocha Brendan Rodgers katika Uwanja wa Anfield ni bonge la kamari.
Rodgers, ambaye aliiongoza Swansea kushika nafasi ya 11 kwenye Ligi Kuu msimu uliopita, anasaini mkataba wa miaka mitatu Liverpool.
"Ni bonge la kamari kwa kuteuliwa kwake na kamari kubwa ambayo klabu haijawahi kucheza kwa muda mrefu," alisema Lawrenson.
"Mashabiki wa Liverpool watampa nafasi. watampa muda. Lakini kama timu haitamaliza ndani ya nne bora, wamiliki watafanyeje?"
Rodgers amewahi kuzifundisha Reading na Chelsea kabla ya kwenda Watford Novemba mwaka 2008.
Alipoulizwa kuhusu sifa za kocha huyo mwenye umri wa miaka 39, Lawrenson alisema: "Rodgers amefanya kazi nzuri akiwa Swansea, kila mmoja anapenda jinsi wanavyocheza soka yao.
"Nafasi ya Brendan kuongoza klabu ambayo ipo ndani ya 10 bora nchini ipo juu ya uwezo wake. Ni changamoto tofauti kwake, klabu itatarajia kushinda kila mechi.
"Liverpool ilitumia fedha nyingi katika usajili msimu uliopita, hakuna shaka watatumia fedha nyingi zaidi. Ni kazi kubwa kwa Rodgers, kwa sababu atawajibika kwa kila kitu kama ilivyo hakuna Mkurugenzi wa Michezo,"alisema.