SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) linatafakari mustakabali
wa Yanga, kufuatia Wajumbe kadhaa wa Kamati ya Utendaji ya Yanga akiwemo
Mwenyekiti, Wakili Lloyd Baharagu Nchunga kujiuzulu.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace
Wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba, Kamati
ya Uchaguzi ya Yanga imeliandikia barua shirikisho hilo, ikitaka mwongozo juu
ya hilo.
Wambura amesema kwamba, kwa kuzingatia hilo, TFF imepeleka
suala hilo kwa Kamati yake ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ili itoe
maoni yake kisheria ya nini kinafanyike kuhakikisha Yanga inaendelea na
shughuli zake kama kawaida.
Amesema Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji
chini ya Mwenyekiti wake, Alex Mgongolwa (pichani) inatarajia kukutana leo jioni
kushughulikia suala hilo na baadaye Kamati ya Uchaguzi ya Yanga pamoja na
Kamati ya Uchaguzi ya TFF zitapewa maelekezo ya kufanya kwa kuzingatia taratibu
zilizopo.
0 comments:
Post a Comment