• HABARI MPYA

    Monday, May 28, 2012

    MISS DAR INTER COLLEGE MAZOEZINI

    SHINDANO la Miss Dar Inter College 2012 linatarajiwa kufanyika Juni 8, mwaka huu katika ukumbi wa San Sirro, Sinza, Dar es Salaam likisindikizwa na burudani baab kubwa, kutoka kwa wasanii na vikundi ambavyo vitatajwa baadaye, kwa mujibu wa Dina Ismail, Mratibu wa shindano hilo.
    Vimwana 15 wanaendelea na mazoezi, chini ya mwalimu wao, Marylidya Boniphace, Miss Dar Inter College 2009 kwenye hoteli ya Lamada, Ilala mjini Dar es Salaam.
    BIN ZUBEIRY ilitembelea kambi ya warembo hao jioni ya leo, na kukuta totoz zisizopungua nane zikijinoa, wakati warembo wengine walikuwa wana udhuru. Hebu cheki totoz na jiulize kwa njini Juni 8 usiende San Sirro kucheki swaga zao.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MISS DAR INTER COLLEGE MAZOEZINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top